Simanjiro waanza kukeketa watoto wachanga, Madaktari wasema madhara zaidi yataongezeka
Huyu ni ngariba aliyekeketa maelfu ya wasichana katika eneo hilo
Fredy Azzah
WAKATI serikali pamoja na mashirika yasiyo ya
kiserikali kutoka ndani nan je ya nchi yakitafuta njia ya kupambana na
ukeketaji, ndivyo jamii inayoabudu mila hizi potofu wanavyotafutwa njia ya
kutekeleza ukatili huo bila kubainika.
Jamii ya wananchi wa Simanjiro ambayo asilimia
95 ya wakazi wake ni wamasai na waarusha, wamebadili kutoka kufanya ukeketaji
kwa wasicha wenye umri mkubwa uliokuwa ukikadiriwa kuwa 14 mpaka 18 na sasa ni
watoto wadogo wenye wiki moja mpaka
mwezi mmoja.
Nang’urutu Kariayi (49), mkazi wa Narokusoito kata ya Langai, ni ngariba maarufu katika
eneo hilo ambaye alianza kazi yake hiyo zaidi ya miaka 10 iliyopita,
anathibitisha hilo akisema kuwa lengo kuu ni kukwepa kukamatwa na kuweza
kulinda mila za kabila hilo.
“Kwa
siku nakata hata zaidi ya 10 kwa sababu kwa mtu mmoja anaweza akawa ana mabinti
watano, na ile kitu siyo ngumu kwa sababu haina mfupa,” anasema Kariaya baada
ya kutaka kujua idadi ya watoto anaowakeke kwa mwaka.
Anasema wakati masika kwake huwa siyo huwa na
furaha yakupata nvua ya kustawisha mazao yake tu, ila pia ni kipindi cha kupata
fedha kwani wakati huu ndiyo shughuli za
tohara kwa waume na ukeketaji kwa
wasichana ambao watu wa eneo hili wanaujua kwa jina la Emurata Ndito, ndiyo
hufanyika.
“Wakati wa masika ndiyo huwa nakeketa kwa
sababu huwa kuna baridi na damu za watoto zimetulia, hakuna mtu anaangaika
kutafuta majani kwa ng’ombe, kwa hiyo alifajiri tu nakeketa hata zaidi ya 10,”
anasema mama huyo aliyekuwa akizungumza kwa msaada ya mkalumani kutokana nayeye
kutoelewa vizuri kiswahili.
Anasema licha ya kuwa kwa wauname kutahiriwa
hufanyika kwa msimu ili kupata marika mbalimbali, yaani tohara kufanywa kwa
miaka saba mfululizo kasha kusitishwa kwa kipindi cha miaka saba kabla ya
kuanza tena, kwa wanawake ukeketaji huwa hauna msimu.
“Kwa wanake hakuna msimu kwa kuwa watoto
wanakua kila siku, lakini siku hizi huwa unafanyika kwa siri kwa sababu
Serikali haitaki,” anasema mama huyo.
Anasema kuwa, hakuna mtu aliyemfundisha
kufanya kazi hiyo lakini kwa kuwa yeye mwenyewe aliona jinsi alivyokeketwa
kisha kumuona mama yake mzazi ambaye alikuwa ngariba pia akifanya kazi yake,
nay yeye sasa ni fundi wa kufanya shughuli hiyo ambayo kwake ni kazi inayompa
kipato cha kula na watoto wake 10 alioachiwa ma mumewe ambaye kwa sasa ni
marehemu.
“Mimi mwenyewe nimekata ya ndito (wasichana)
yangu nne,” mama huyu ambaye muda wote alikuwa akizungumza msaada wa mkalumani
alieleza maneno hayo mwenyewe huku akionyesha ishara kwa kidole pia.
Hata
hivyo ngariba huyu anasema kuwa, tofauti na zamani ambapo walikuwa
wakikeketewa wasichana ambao walikuwa karibu na kuolewa, siku hizi wanaokeketwa
ni wenye kati ya miaka sita na saba.
“Ukiacha wanakuwa wanapata akili wanakataa
kukeketwa au wakati mwingine wakianza shule wanaingiziwa mambo ya ajabu
yanayowafanya wakae mila zao,” anasema ngariba huyu.
Anasema kazi hiyo aliinza akiwa na watoto
watano na kuwa, zamni walikuwa wakifanya kwa ujira wa kupewa mbuzi kwa kukeketa
mtoto mmoja lakini siku hizi huwa kukeketa mtoto mmoja ni Sh20,000.
Kwa kujiamini mama huyu anakiri kuwa anajua
sharia inakaza ukeketaji lakini anasema kuwa, anaamini hawezi kukamatwani kwani
kukeketa ni mila ya kimasai na hakuna mmasai anayeweza kumsemea kwa vyombo vya
dola mpaka akamatwe.
“Bado wamasai wanapenda mila zao, siyo rahisi
watoke wakaseme kuwa kuna mtu anakeketa, ukweli hakuna masai asiyekeketa, hata
hao wa mjini wapo ambao huwa wanarudisha watoto wao huku nakuja kuwa keketa,”
anasema mama huyo.
Ngariba huyu anaenda mbali zaidi kusema kuwa,
hata viongozi wa vijiji hawawezi kufanya lolote kwani, wenyewe pia wanampelekea
watoto wao ili awakekete.
Ngariba huyu anasema, sababu kubwa inayofanya
vitendo hivi kuendelea katika jamii ya kimasai, ni kulinda mila za kabila hilo.
Anasema pia kuwa, sababu nyingine ni za kiafya
ambapo hukeketa watoto ama hata watu wazima wakiwa wanaumwa ugonjwa alioutaja
kwa jina la lawalawa.
Anasema kuwa, hata kama mtu amesha keketwa
akiumwa tena ugonjwa huu wa lawalwa, huchanjwa sehemu zake za siri haswa maeneo
ambayo yameathirika sana kasha kuwekewa dawa za kienyeji.
“Hii dawa ni chungu, lakini tumekuwa
tukiitumia muda wote na watu wanapona,” anasema.
Hata hivyoMganga Mkuu wa Hospitali ya
Orkesment anasema ugonjwa huo wa lawalawa kitaalam unajulikana kwa jina la
Urinary tract infection ama kama wengi walivyo zoea kuuita (UTI).
Dk Loishorua Ole Yamat anasema kuwa, anasema
kuwa watoto wengi na hata baadhi ya watu wazima huugua ugonjwa huo kutokana na
kukaa uchafu.
“Utakuta wanafunika watoto na nguo chafu,
hawawafanyii usafi wa kutosha, sasa wakiuguwa huo ugonjwa wao wanawakeketa,
lakini UTI ni ugonjwa ambo unatibika hospitali kiurahisi tu, ndani ya wiki moja
unameza dawa unapona,” anasema Dk Ole Yamat.
Anasema kuwa, mara nyingi jamii ya eneo hili
imekuwa ikishikilia imani hiyo kwa muda mrefu sasa huku akisena kuwa, hatua
ambayo jamii hiyo imefikia ya kuwakeketa watoto wadogo inaongeza mazara ya
kitendo hicho mara dufu.
“Ukimkeketa mtoto mdogo unaongeza hatari ya kumwambukiza
maradhi mengine kwa kuwa bado kinga yake ipo chini siyo kama mtu mzima, lakini
pia hata wakati wa kumkeketa anaweza kuumia sana kwa sababu ya kuangaika
kutokana na maumivu atakayo sikia,” anasema Dk Ole Yamat.
Jacobo Lemburis mkazi wa Orkasmenti anasema
kuwa, licha ya eleimu kusambazwa katika eneo hilo juu ya madhara ya
ukeketaji wananchi hao wamekuwa wagumu
kuachana na vitendo hivyo.
Anasema licha yam zee aliyemtaja kwa jina la
Ngatai Lepilali mkazi wa eneo hilo kukeketa mtoto na kupoteza maisha, bado
wanajamii wa eneo hilo hawajapata funzo.
“Badala ya kuachana na hali hiyo sasa
wanakeketa watoto wadogo,” anasema.
Lemburis naye anaungana na Ngariba Kariaya kwa
kusema kuwa, ukeketaji hufanyika zaidi wakati wa masika huku yeye akitoa sababu
ya kuwa na mifuho iliyonona kuwa ni moja ya sababu ya wakati huo kutumika zaidi
kwa shughuli hiyo.
“Wakati wa masika utakuta mifugo imenona kwa
hiyo waliokeketwa hawakosi chakula, na watu wanakuwa hawangaiki kwa shida ya
maji wala chakula kwa mifugo,” ansema Lemburis.
Anasema kuwa, sababu za kuwakeketa ni ili
wasiwe Malaya, na pia wawe na busara.
“Kwa masai mwanamke ambaye hajakeketwa hata
kama ana miaka mingapi, yeye anaonekana tu kuwa ni mtoto mdogo na hana busara
yoyote,” anasema Lemburis.
Anasema kuwa, katika eneo hilo hawezi kusema
kuwa vitendo hivyo vimepungua kwani ila ni kuwa stahili imebadilika kutoka
kukeketwa kwa sherehe na kufanya siri.
Anaeleza pia kuwa, kukomeshw kabisa kwa hali
hiyo kunakuwa kugumua kutokana na mangariba kufanya shughuli hiyo kama kazi yao
ya kuwapatia kipato.
Naye Martha Okida ambaye ameshawahi kufanya
shughuli za uhamasishaji ili watu waachane na tabia hiyo, anasema bado hali ni
mbaya sa.a
“Tuliwahi kwenda katika shule mbalimbali za
msingi, ukiwapa watoto karatasi waandaike kama wamekeketwa ama laa, kuanzia
darasa la kwanza mpaka la tatu tu, unaweza kukuta watano tu ndio hawajakeketwa,
na wanakwandikia mpaka majina ya mangariba walio wakeketa,” anasema Okida.
Mama huyu pia anasema kuwa, wanasiasa kwa
kiasi kikubwa wanakuwa na kigugumizi kukemea vitendo hivyo kwa kugopa kupotea
nyadhifa zao.
Naye Naishie Saitoti Mkazi wa Kijiji cha
Langai anasema kuwa, kuacha mila hiyo ni vigumu huku akisema siyo wamasai pekee
wanaokeketa.
“Kwani sisi tuache, mbona kuna makabila mengi
tu wanakeketa, bibi zetu walikeketwa na mama zetu lakini walituzaa, kwanini
sisi tusiwakekete watoto wetu,” anasema mama huyo.
Wati utafiti uliofanywa na Mwananchi kwa ushirikiano na Tamwa ukibaini hayo,baadhi
ya wanasiasa wakiwamo madiwani na wenyeviti wa vijiji, wanasema kwa kiasi
kikubwa hali ya ukeketaji haipo kwenye maneo yao.
Diwani wa kata ya Orkasiment Naftal Samuel,
anasema kuwa katika eneo lake hajawai kuona vitendo vya ukeketaji vikifanyika
kwa muda mrefu sasa hali inayomfanya aamini kuwa vitendo hivyo vimepungua kwa
kiasi kikubwa.
“Zamani ilikuwa ni rahisi kujua kama kuna
watoto wanakeketwa kwa sababu kulikuwa na sherehe kubwa tu zinafanyika watoto
wakikeketwa lakini siku hizi hakuna hayo mambo,” anasema Samuel.
Naye Diwani wa Langai Jackson Lesikari anasema
kuwa, kwa kiasi kikubwa vitendo hivyo ktika eneo lake havipo, na kuwa wananchi
wamebadilika baada ya kupatiwa elimu juu ya madhara ya vitendo hivyo.
“Ukeketaji wameacha kabisa baada ya kipewa
elimu, watu wanaotoa elimu wanashirikiana na malaigwanani (vaiongozi wa kimila
wa kimasai),” anasema Lesikari
Anasema kuwa, shirika lisilokuwa la kiserikali
la Nafgem, linalotoa elimu juu ya ukeketaji, kwa kiasi kikubwa limefanikiwa
kupunguza tatizo hilo kwa wanajamii hao.
Mwenyekiti w Kijiji cha Lolumorijei Jeremia Lemandi,
anasema kuwa katika eneo lake vitendo vya ukeketaji vimepungua huku akisema
kuwa, kwa kiasi kikubwa wanawake ndiyo wanaojua ukweli wa vitendo hivyo kwani
ndio huvitekeleza.
“Wakinamama ndiyo wanakeketa, ukiwauliza ndiyo
watakwambia vizuri,’ Lemandi.
Ingawa Lemandi anasema hayo, watu mbalimbali
wa eneo hili wanasema kuwa, mtoto ni mali ya baba na wala mama hana sauti
yoyote juu yake na hivyo baba ndiye mwamuzi wa kila jambo kwa binti yake ikiwa
ni pamoja na kuamua akeketwe aole na mambo mengine kam hayo.
Naye Naomi Meshilieki anasema kuwa, kwa kiasi
kikubwa wanafunzi ambao wanaingia shuleni bila kukekeketwa, hufanyiwa vitendo
hivyo wakati wa likizo ama wakati mwingine kusingia shuleni kuwa wanaumwa.
Mkuu wa Shule ye Simanjiro Jacobo Khahima anasema kuwa, ni vigumu kuainisha madhara ya
ukeketaji kwenye elimu kwa kuwa vitendo hivyo hufanyika kwa usiri mkubwa.
Lakini Ofisa Elimu Msingi wa Wilaya hiyo Jackson Mbise, anasema kwa kiasi kikubwa
vitendo hivyo vinachangia katika kudidimiza elimu katika eneo hilo.
Anasema kuwa, sababu zinazochangia hali hiyo
ni mafunzo ambayo mabinti hupewa wakati wa kukeketwa ambayo huwafanya kujiona
kuwa ni watu wazima na wanaweza kufanya chochote.
“Wakitoka huku wanakuwa tayari wameondolewa
kwenye mazingira ya kishule shule, wanajiona sasa wao ni watu wazima wapo
tayari kutembea na wanaume na kujenga familia, elimu kwao huwa ni kitu kidogo
sana,” anasema.
Anasema kuwa, hali hiyo ndiyo sasa husababisha
mimba na wengine kuacha shule na kuolewa, mambo ambayo kwa ujumla wake anasema
yanaporomosha elimu katika eneo hilo.
Mrakibu wa Polisi Wilaya ya Simanjiro (ASP)
Felix Kikwala, anasema kwa kiasi kikubwa kuwakamata watu wanaotekeleza vitendo
hivyo noi vigumu kwani vinafanyika kwa usiri wa hali ya juu.
Kwa upande wake Ofisa Mradi wa Shirika
linalotoa Elimu Juu ya Madhara ya ukeketaji Nafgem, Michael Nyari, anasema kwa
kiasi kikubwa wanetoa elimu katika jamii ya eneo hilo juu ya madhara ya vitendo
hivyo.
Anasema moja ya changmoto wanayokabiliana nayo
nikuwa, jamii ya kimasai inaheshimu sana vitendo vya ukeketaji hivyo wakati
mwingine inauwa vigumu kuacha kabisa mila hizo.
“Wamasai ni watu wenye siri sana, wanatekeleza
hivi vitendo sasa katika hali ya usiri na hata hao wanaofanyiwa kati ya mambo
wanayofundishwa ni kuwa wasiri na kutunza mila zao, wanaamini wakizivunja
wanaweza kulaaniwa hata wakapoteza maisha,” anasema Nyari.
Moja ya mambo yanayoelezwa kuwa yanaweza
kukomesha vitendo hivyo ni pamoja na mangariba kupewa njia nyingine ya
kuendesha maisha yao kwani wengi wamefanya shughuli hiyo kuwa ni mired.
Jambo linalothibitishwa na Ngariba Kariayi
anayesema kuwa, shughuli ya ukeketaji ndiyo inayomuwezesha kutunza watoto 10
alioachiwa na marehemu mume wake.
“Sasa hivi kwanza mimi nimeshakuwa hata
mkirsto, nikiweza kupata kitu kingine cha kufanya nitaachana hata hii kazi,”
anasema ngaiba huyo.
Hata hivyo pia wanasiasa wanatakiwa kubadilika
na kuwa na ujasiri wa kukemea vitendo hivyo badala ya kuwa na sura tofauti
katika kutekeleza vita dhidi ya vitendo hivyo.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa
Halamashauri ya Wilaya hiyo Patrick Saduka, anasema kuwa kwa sasa wanafanya
uchunguzi ili kujiridhisha kama kweli kuna vitendo vya ukeketaji kwa watoto.
“Tulikuwa na kikao hivi karibuni tukishauriana
jinsi ya kujiridhisha na taarifa zilizopo, tulifikiri labda watoto wakija
kiliniki wakaguliwe lakini tukaona kuna changamoto zake, kwa hiyo bado
tunaumiza kichwa kuangalia jinsi ya kubaini hilo,” anasema Saduka.
Anasema pia kuwa, katika kupambana na suala
hilo mmoja wa ofisa wa Halmashauri hiyo anashirikiana kwa ukaribu na shirika
lisilo la kiserikali la Nafgem ili kupata maelezo ya kina juu ya ukubwa wa
tatizo hilo.
No comments:
Post a Comment