Saturday, July 14, 2012


Mwalimu wa madrasa alivyonajisi
wasichana wanne, wavulana wawili  
NI WA MIAKA MIWILI HADI 10, SHEIKH AKEMEA ASEMA
MEZANI KWAKE YAPO MASHAURI SITA YA NAMNA HIYO

Fredy Azzah
MATUKIO yanayofanywa na baadhi ya binadamu, yanaweza kufanya waamini wa dini mbalimbali kuamini kuwa kiama kimekaribia.Kwa kiasi kikubwa vitendo hivi ambavyo vipo kinyume kabisa na ubinadamu, vinatekelezwa na wale waliotarajiwa kuvikemea, huku wakiwa wamejificha na kivuli cha vyeo vyao.