
Fidelis Butahe
KATIKA hali isiyo ya kawaida watoto wenye umri chini ya miaka 18 wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali au waliohukumiwa huwekwa sehemu moja na watu wazima katika Gereza la Segerea, jijini Dar es Salaam jambo ambalo limesababishia baadhi yao kuingiliwa kinyume na maumbile na kuharibiwa vibaya.Tuhuma hizo nzito dhidi ya magereza zilibainika wakati Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi, ilipokuwa ikieleza mambo mbalimbali iliyoyakuta katika gereza hilo baada ya kufanya ziara, mbele ya wajumbe wa Kamati hiyo ya Mambo ya Nje ulinzi na usalama inayoongozwa na Waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa.