Monday, September 12, 2011

watanzania wanaanza ngono mapema sana.

Fredy Azzah

IMEBAINIKA  kwamba Watanzana wanaanza kufanya ngono wakiwa na umri mdogo zaidi hali inayosababisha kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi pamoja na idadi ya watu kuongezeka.

Takwimu zilizotolewa jana jijini Dar es Salaam na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Idadi ya Watu (UNFPA), katika kongamano la Afya ya Uzazi kwa vijana, lililokutanisha makundi mbalimbali ya vijana, zilieleza kwamba wasichana ni  kundi lililoathirika zaidi.

Ofisa Mipango wa Ukimwi wa UNFPA Dk Chilanga Asmani, alisema takwimu za shirika hilo zinaonyesha kwamba asilimia 59 ya wasichana huanza ngono wakiwa na chini ya miaka 18 huku ikiwa ni asilimia nne ya vijana wanaoanza ngono wakiwa chini ya umri huo.