Anthony Mayunga-Serengeti
MKAZI mmoja katika mtaa wa NHC mjini Mugumu Samson Kitoshi (32) amekufa baada ya kujinyonga kwa kamba chumbani kwake kwa kile kilichodaiwa kuwa amechoka kupigwa na mkewe kila wakati.
Tukio hilo limevuta umati mkubwa wa watu linadaiwa kutokea Agosti saba saa tano asubuhi chumbani kwake alipofunga kamba juu ya dari na kuning'inia hadi alipokata roho.
Akisimulia mkasa huo mtoto wa marehemu Rehema Samson (10) anayesoma darasa la 3 shule ya msingi mapinduzi alisema kabla ya kutokea kwa tukio hilo mama yao alimpa Sh 1,000 anunue sukari na vitafunio, lakini asimpe baba yao chai.